katiba yaTYEC











i
Yaliyomo
Ibara Maelezo ukurasa
SEHEMU YA KWANZA ..........................................................................................................................................1
UTANGULIZI ........................................................................................................................................................1
JINA, MAKAO MAKUU YA JUMUIYA, ITIKADI, LUGHA, BENDERA, NEMBO ......................................2
5. BENDERA YA JUMUIYA ...............................................................................................................................2
6. NEMBO YA JUMUIYA ...................................................................................................................................3
SEHEMU YA PILI.....................................................................................................................................................3
MISINGI NA MADHUMUNI YA JUMUIYA .....................................................................................................3
7. MISINGI YA JUMUIYA ...................................................................................................................................3
8. MADHUMUNI YA JUMUIYA .........................................................................................................................4
SEHEMU YA TATU .................................................................................................................................................6
UANACHAMA KATIKA JUMUIYA ..................................................................................................................6
9. UANACHAMA ..................................................................................................................................................6
10. HAKI ZA MWANACHAMA ..........................................................................................................................7
11. WAJIBU WA MWANACHAMA....................................................................................................................8
12. MWISHO NA UHALI WA KUWA MWANACHAMA ................................................................................8
SEHEMU YA NNE ....................................................................................................................................................9
UONGOZI WA JUMUIYA ...................................................................................................................................9
14. VIPIMO VYA KIONGOZI KATIKA JUMUIYA...........................................................................................9
15. HAKI ZA KIONGOZI .................................................................................................................................. 10
16. KUACHIA UONGOZI /KUACHA MADARAKA ...................................................................................... 10
SEHEMU YA TANO .............................................................................................................................................. 11
VIKAO VYA JUMUIYA/NAMNA MPANGILIO WA VIKAO VYA T.Y.E.C............................................... 11
17. NGAZI YA KATA/SHEHIA ........................................................................................................................ 11
1. MAJUKUMU YA KAMATI YA UTENDAJI KATA/ SHEHIA .................................................................. 11
2. WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA KATA ....................................................................................... 12
3. KAZI ZA MKUTANO MKUU NGAZI YA KATA ..................................................................................... 12
4. KAZI ZA MWENYEKITI WA KATA/SHEHIA ........................................................................................... 13
5. KAZI ZA KATIBU WA KATA /SHEHIHA .................................................................................................. 13
6. KAZI ZA MWEKA HAZINA WA KATA/SHEHIA ..................................................................................... 13
18. NGAZI YA WILAYA ................................................................................................................................... 14
ii
1. WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA WILAYA .................................................................................. 14
2. KAZI ZA MKUTANO MKUU WA WILAYA ............................................................................................. 14
3. KAZI ZA WAJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI YA WILAYA ..................................................... 15
4. KAZI ZA KAMATI YA UTENDAJI YA WILAYA .................................................................................... 15
5. KAZI ZA MWENYEKITI WA WILAYA ..................................................................................................... 16
6. KAZI ZA KATIBU WA WILAYA ................................................................................................................ 16
7. KAZI ZA MWEKA HAZINA WA WILAYA ................................................................................................ 16
19. NGAZI YA MKOA ....................................................................................................................................... 17
1. WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA MKOA; ................................................................................ 17
2. MAJUKUMU YA MKUTANO MKUU WA MKOA. ............................................................................... 17
3. KAMATI YA UTENDAJI YA MKOA HUUNDWA NA WAJUMBE WAFUATAO. ................................ 17
4. KAZI ZA KAMATI YA UTENDAJI YA MKOA .................................................................................... 18
5. KAZI ZA MWENYEKITI WA MKOA ................................................................................................... 18
6. KAZI ZA KATIBU WA MKOA ............................................................................................................... 18
7. KAZI ZA MWEKA HAZINA WA MKOA. .............................................................................................. 19
20. NGAZI YA TAIFA ..................................................................................................................................... 19
1. WAJUMBE WATAKAO WAKILISHA KWENYE MKUTANO MKUU WA TAIFA. ......................... 19
2. KAZI ZA MKUTANO KUU WA TAIFA. ................................................................................................ 20
3. WAJUMBE WA KAMATI KUU TAIFA. ................................................................................................ 20
4. KAZI ZA KAMATI KUU YA TAIFA (JUMUIYA) ................................................................................. 20
21. KAMATI KUU MAALUMU (ZANZIBAR) ................................................................................................ 21
1.WAJUMBE WA KAMATI MAALUMU YA (KAMATI KUU TAIFA) ................................................... 21
2. KAZI ZA KAMATI MAALUMU YA KAMATI KUU YA TAIFA. ........................................................ 22
SEHEMU YA SITA ................................................................................................................................................ 22
22. SEKRETARIETI YA JUMUIYA ................................................................................................................. 22
23.SEKRETARIETI YA JUMUIYAYA KAMATI MAALUM YA KAMATI KUU YA TAIFA. ................... 23
SEHEMU YA SABA .............................................................................................................................................. 24
24. VITENGO VYA JUMUIYA. ........................................................................................................................ 24
SEHEMU YA NANE ............................................................................................................................................. 24
25. BARAZA LA WADHAMIANI LA JUMUIYA . ...................................................................................... 24
SEHEMU YA TISA ................................................................................................................................................ 26
26. VIONGOZI WAKUU WA JUMUIYA NA NAFASI ZAO KATIKA JUMUIYA ...................................... 26
1. MWENYEKITI /RAIS WA JUMUIYA TAIFA. ........................................................................................... 26
iii
2. MAKAMU WENYEVITI TAIFA .................................................................................................................. 27
3. KATIBU MKUU. ........................................................................................................................................... 27
4. NAIBU MAKATIBU WAKUU. .................................................................................................................... 28
5. MWEKA HAZINA TAIFA. .......................................................................................................................... 28
SURA YA KUMI .................................................................................................................................................... 28
MAMBO MENGINE YAHUSUYO JUMUIYA. ............................................................................................... 28
27. UCHAGUZI. ................................................................................................................................................. 28
28. AKIDI ZA VIKAO. ....................................................................................................................................... 28
29. UITISHAJI WA VIKAO VYA JUMUI YA. ................................................................................................ 29
30. MJUMBE AWEZA KUPOTEZA UJUMBE KAMA. ................................................................................. 29
31. RATIBA ZA VIKAO ................................................................................................................................... 29
32. ANAYE KAIMU MADARAKA ................................................................................................................. 29
33. KURA ZENYE KUHITAJI UAMUZI......................................................................................................... 29
34. KAMATI YA NIDHAMU NA USULUHISHO. ......................................................................................... 30
35. VITENGO NA TAASISI ZA JUMUIYA. ................................................................................................... 30
36. MABADILIKO /MAREKEBISHO YA KATIBA HII. ............................................................................... 30
37. JUMUIYA KUINGIA MSETO NA ASASI ZINGINE. .............................................................................. 30
38.KUVUNJIKA NA MWISHO WA JUMUIYA .............................................................................................. 31
iv
1
SEHEMU YA KWANZA
UTANGULIZI
Kwa vile Tanzania ni nchi yenye makundi mbalimbali ya watu yanayowiana na kutofautiana kwa dini, elimu, itikadi, kipato na fikra. Lakini bado tatizo la ajira, thamani ya kutambuliwa bado ni tatizo kubwa katika jamii zetu hususani kwa kundi la watu walio wengi na wenye kipato cha chini kama vijana ni lazima makundi haya makubwa likiongozwa na vijana waungane kama namna ya kujenga hoja ya pamoja kufikia malengo yao.
Kwa vile kutothaminika katika maswala ya ajira pamoja na misingi ya kitaifa na kimataifa vijana wengi wamekata tamaa hadi kufika hatua ya kutoshiriki kikamalifu kwenye ujenzi wa jamii zao na taifa kwa ujumla na kwa vile matatizo haya yameletwa na rushwa na washirika wake wakubwa kama vile vibaraka wasioweka mbele maslahi ya taifa, ndugu zao na wa kuanza kusaliti tamaduni zao, tatizo la ufisadi na rushwa iliyokomaa bado imeonekana kushika kasi katika jamii zetu na zaidi kuwaathiri wasiojiweza na tabaka kubwa la vijana zaidi ya asilimia sabini kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2002.
Na kwa vile TYEC ni jumuiya ya kiraia na taasisi isiyo ya kiserikali inayoamini katika utu na ubinadamu ndani na nje ya Tanzania na kwa vile TYEC imejengwa katika misingi ya nidhamu uzalendo na na mshikamano katika kuboresha maisha ya vijana na zaidi kuhamasisha kujituma kwa vijana katika kujiletea maendeleo ya mtu binafsi na taifa kwa ujumla.
Na kwa vile TYEC inatambua kwa dhati swala la ujira na ambalo linaonekana kusumbua zaidi vijana wanaohitimu masomo katika ngazi mbalimbali na kushidwa kupata ujira wao kwa wakati na usahihi. TYEC sasa imedhamiria kwamba, kwa kushirikiana na serikali, asasi za kiraia na zisizo za kiraia, taasisi za dini pamoja na serikali kuu kutafuta namna ya kuwaunganisha vijana ili kufikia malengo yao kama ilivyokuwa dhamira yao ya kutafuta elimu katika taasisi mbalimbali.
Na kwa kuwa malengo sahihi ya TYEC ni kuwaunganisha vijana wasomi mbalimbali na katika taasisi mbalimbali waweze kujenga maisha yao binafsi na taifa kwa ujumla, TYEC itashirikiana na chombo chochote chini ya misingi na madhumuni ya jumuiya hii kwa lengo la kuwaunganisha vijana, kujiletea maendeleo yaobinafsi na taifa kwa ujumla.
2
Hivyo basi sisi wana TYEC kwa pamoja tunapitisha katiba hii leo12 Juni 2012 mjini Arusha kuwa fimbo na muongozo wa shughuli na taratibu za jumuiya kwenye mkutano mkuu maalum wa jumuiya
JINA, MAKAO MAKUU YA JUMUIYA, ITIKADI, LUGHA, BENDERA, NEMBO
1. Jumuiya hii itaitwa TANZANIA YOUTH ELITE COMMUNITY (T.Y.E.C).Yenye maana ya Jumuiya ya Vijana Wasomi Tanzania.
2. Makao makuu ya jumuiya yatakuwa mjini Arusha na makao madogo ya jumuiya yatakuwa huko mjini Zanzibar.
3. Itikadi ya jumuiya ni utu na ubinadamu unaotafuta heshima na kutambulika kwa madaraja mbalimbali ya watu katika jamii.Na kwamba utu wa binadamu hauwezi kununuliwa wala kufananishwa na kitu kingine chochotete zaidi ya kuthamiwa kutambuliwa na kuheshimiwa.
4. Lugha rasmi itakayo tumika kuwaunganisha wasomi na makundi mengine katika Tanzania itakuwa kiingereza na kiswahili.
5. BENDERA YA JUMUIYA
Bendera ya Jumuiya itakuwa na rangi kuu Tatu, Rangi ya kwanza itakuwa (Nyekundu yenye utambuliso wa upendo wa dhati wa vijana wasomi kwa Taifa lao. Rangi hizi zinatambua kuwa upendo bila matendo ni sawa na bure tena usaliti, hivyo kwa rangi hii vijana wanapania kuudhatiti upendo kwa Taifa kwa njia dhabiti ya matendo na kujishughulisha kama njia ya kujenga Taifa la kujitegemea.
Rangi ya pili ni nyeupe ikiwa maana ya Amani kabambe iliyo Tanzania, Amani hii iliasisiwa na viongozi wazalendo waliolileta taifa hili kwenye mikono ya watanzania walio wengi japo, walioasisi amani hivi kwa wengi wao hatunao tena hivyo basi vijana wanapania kuizatiti amani hii kwa njia ya (kuungana) pale pote walipo, kwa kuunganisha mawazo, katika vyanja za uchumi, siasa, na kijamii ili kuleta mageuzi kwa vijana na Taifa kwa ujumla (hii ndiyo) njia pekee ya kuuasisi amani iliyopo Tanzania.
Rangi ya Tatu ni ya njano, ikiwa na tafsiri ya rasilimali lukuki tulizojaliwa kuwa nayo sisi waTanzania, kama vile misitu, Ardhi kubwa, vyanzo vya maji na milima ijapokuwa rasilimali hizi hazijaweza kudhihirisha maana yake kwa muda wa miaka mingi ikiwa na maana ya kufuta umasikini kwa wa Tanzania. Vijana wanaazimia kuungana kwa pamoja chini ya Jumuiya moja kushirikiana na Serikali
3
kubuni namna ya kutumia rasilimali hizi kwa namna ya kumnufaisha mtanzania kijana msomi na jamii yake kwa upana. Kwamba matumizi yake lazima yahitaji ushirikiano mkubwa kwa manufaa ya kizazi cha leo na kesho hii ndio namna pekee ya kunufaika na raslimali zetu.
6. NEMBO YA JUMUIYA
Nembo ya Jumuiya itakuwa na vitu vifuatavyo / Nembo zifuatavyo: katikati kutakuwa na mwenge wenye maana ya mwangaza, mwangaza huo ni vijana wanaounda nguvu kazi kubwa ya Taifa la Tanzania. Kwenye shina la mwenge kutakuwa na mkono kila upande ukiwa na maana ya nguvu ya vijana katika ujenzi wa Taifa kupitia matumizi yakinifu ya raslimali zilizopo Tanzania. Kila upande wa mwenge kutakuwa na rangi za bendera ya Taifa letu Tanzania, ikiwa na maana ya vijana ndani ya Taifa la Tanzania. Na nyuma ya mwenge kuna bendera ya jumuiya ya vijana wasomi wa Tanzania, ikiwa na maana ya mahusiano ya vijana na maendeleo ya Taifa la Tanzania. Juu ya mwenge kuna maneno ya kiingereza yasemayo Tanzania Youth, Elite Community kwa kifupi T.Y.E.C ikiwa na Tafsiri yake chini kabisa ya mwenge yenye maana ya jumuiya ya vijana wasomi Tanzani kauli mbiu ya Jumuiya hii ni vijana tunaliangaza Taifa. Na itikadi yake itakuwa Utu na Ubinadamu.
SEHEMU YA PILI
MISINGI NA MADHUMUNI YA JUMUIYA
7. MISINGI YA JUMUIYA
1. TYEC.itaheshimu na kutambua fikra zinazotolewa na makundi mbalimbali kwa namna ya kujenga jumuiya ya vijana.
2. Utu na ubinadamu ndio kitambulisho kikuu itakayoitambulisha (tyec) ndani ya jamii ya Tanzania na nje ya mipaka yetu.
3. Kuthamini mchango wa wanachama na wasio wanachama yanayoletwa katika jumuiya kama njia ya kusaidia vijana na makundi mengine kujikomboa kwenye umaskini.
4. Kushirikiana na makundi mengine katika jamii chini ya itikadi ya jumuiya pamoja na misingi ya (TYEC).
4
5. Kushirikiana na jumuiya nyingine zote kutangaza uhalali wa haki za binadamu katika yanja za siasa, uchumi na kitamaduni ikiwa ni ndani na nje ya Tanzania
6. Kuishi katika misingi ya demokrasia katika shughuli zake zote za kila siku kama nyezo muhimu ya kuwakomboa vijana na makundi mengine katika jamii.
7. TYEC, inaamini kuwa ruswa ni mdudu mbaya na hatari katika kuwaunganisha vijana na makundi mengine katika jamii kisiasa kijamii na kiuchumi
8. Tyec, itatambua nakuasisi michango wa wanaharakati mbalimbali wa ukombozi na maendeleo katika Tanzania.
9. Uzalendo na ujasiri ndiyo kitambulisho cha kijana yeyote mtaka mapinduzi na mabadiliko ya kweli katika Tanzania.
10. Afrika ni moja na kwamba TYEC itaungana na Taasisi zingine zote zenye mitizamo sawa kutetea na kusimamia utamaduni wa mwafrika.
8. MADHUMUNI YA JUMUIYA
1. Kudhihirisha thamani ya elimu kupitia kipato kwa wanachama watakaojiunga na jumuiya.
2. Kushirikiana na taasisi zingine zote kuimarisha kilimo ikiwa ni uti wa mgongo wa mwafrika .Hasa kwenye kumwinua kijana msomi wa kiafrika.
3. Kutoa mikopo kwa wanachama kama namna ya kuboresha maisha yao binafsi kufikia maisha bora.
4. Kutunza mazingira kupitia kampeni mbalimbali ikiwa mazingira ni uhai wa mwanadamu.
5. Kutoa fursa za ajira kwa wanachama na makundi mengine ndani ya jamii kama namna ya kuboresha maisha yao.
6. Kuwa daraja lakuwafanikisha wanafunzi wenye ndoto za kupata elimu bora kwenye ngazi ya msingi na sekondari kama namna ya kuyafikia, malengo yao.
7. Kufanikisha malengo kwa wanafunzi wanaojiuga na vyuo mbalimbali kupata elimu na baadaye kuwa nguvu kazi ya taifa la Tanzania.
5
8. Kuhakikisha kuwa TYEC, inakuwa shule ya kuzalisha makada wazalendo watiifu na wenye kuubeza utegemezi.
9. Kutengeneza mlango mrahisi kwa taasisi za serikali na zisizo za serikali ili kuwafikia watanzania kutoa elimu na uhisani wa namna mbalimbali.
10. Kushirikiana na asasi za kiraia kutunga sera kwa idhini ya serikali itakayo simamia rasilimali na kuwanufaisha watanzania maskini kwa fursa ya moja kwa moja.
11. Kushirikiana na vyombo vya dola kutetea haki za watoto na makundi maalum katika jamii waweze kujielimisha na kujiinua kiuchumi.
12. Kutangaza vita waziwazi dhidi ya ubaguzi, udini ukatili na udhalilishaji wa binadamu ndani ya madhari ya Tanzania na nje.
13. Kushirikiana na vyombo vya habari kuhusu vipi watajinufaisha na kujikomboa kutoka kwenye wimbi la umasikini.
14. kuwa na ushirika wa ndani na nje ya nchi kama namna ya kubadilishana mbinu mbalimbali za uzalishaji ,uongozi na na zaidi sana mawasiliano.
15. Kuwasaidia wanaotaka kujiboresha zaidi kielimu, kiuchumui kwani ndio namna pekee ya kutengeneza taifa linalo jitegemea.
16. TYEC,kupitia idara zake mbalimbali itatunga sera na kanuni zenye kuratibu na kutoa ufumbuzi wa maswala kadha wa kadha.
17. Japo TYEC, imejikita kwenye kuwainua vijana wasomi watanzania lakini pia itajikita kwenye kujenga uhusiano imara kwenye jamii ikiwamo ajira na uhamasishaji.
18. kwamba ikishirikiana na taasisi zingine za kitanzania kutangaza Tanzania kama sehemu bora muhimu kwa kuishi,kujipatia elimu na kivutio muhimu kwa wageni kuja kuwekeza kwa manufaa ya taifa na watu wake.
19. Kuwaandaa vijana wa Tanzania kiuchumi na kitamaduni pindi wanapostaafu katika maeneo mbalimabali wasipatwe na changamoto sisizo za lazima.
6
20. TYEC, inaadhimia kuwafanya vijana kufanya shughuli zao za kimaendeleo kwa teknologia ya juu.
SEHEMU YA TATU
UANACHAMA KATIKA JUMUIYA
9. UANACHAMA
Kwa vile Tunatizamia kwa dhati yetu kujenga taifa la wazelendo na imara kiuchumi kwa watu wake,kwa yeyote anayetaka kwa ushawishi wake mwenyewe kujiunga na T.Y.E.C afikie vigezo vifuatavyo ili awe mwanachama halali wa T.Y.E.C
1. Itamfaa awe ni mtanzania kuanzia miaka kumi na sita hadi arobaini na tisa anaye tambulishwa kwa pande zote mbili za muungano, yaani Tanzania bara na Tanzania visiwani.
2. Awe ni mtanzania asiyepungua miaka kumi na sita na asiyezidi miaka arobaini na tisa (16-49).
3. Awe ni mtanzania anayeunga mkono itikadi ya jumuiya ya utu na ubinadamu.
4. Pindi atakapo kuwa mwanachama wa T.Y.E.C atalazimika kununua kitambulisho /kadi ya jumuiya
5. Mwombaji atalazimika kuichukia rushwa na kuubeza utegemezi wa kijana.
6. Mwombaji awe anapenda demokrasia na msatri wa mbele kuunga mkono maswala ya msingi yanayowahusu vijana na makundi mengine katika jamii.
7. Apende kujitegemea na apende ushirikiano na makundi mbalimbali ya watu katika jamii kama njia ya kukomboa wengine.
8. Awe ni Raia wa Tanzania /Mtanzania.
9. Kama ni mtanzania anayeishi nje ya nchi, itamlazimu kulipa ada na michango mengine yote itakayo elekezwa na mamlaka husika ya T.Y.E.C.
10. Awe mzalendo na jasiri wa kuutukuza uafrika na tamaduni zake.
11. Apende kujitolea kwenye maswala ya maendeleo na apende kusaidia wasiojiweza.
12. Awe tayari kufanya kazi popote atakapo elekezwa na mamlaka ikiwa ni namna ya pekee ya kuwaendeleza vijana na watu wengine katika Tanzania.
7
13. Awe walau na elimu ya msingi.
10. HAKI ZA MWANACHAMA
1. Mwanachama atachagua na kuchaguliwa katika nafasi mabimbali za uongozi.
2. Kupewa kwa usahihi taarifa zote zinazohusu jumuiya, ambazo zimejadiliwa na kutolewa maamuzi kwenye vikao vya jumuiya.
3. Ni haki ya mwanachama kwa katiba hii kupata habari mbalimbali zinazohusu jumuiya ndani na nje ya eneo husika ,ilimradi asivunje katiba hii.
4. Mwanachama atasikilizwa na uongozi husika wa jumiya na kuruhusiwa kujitetea mbele ya chombo chochote cha T.Y.E.C kabla ya kuadhibiwa
5. Haki ya kutoa maoni, kusahihisha, kuboresha fikra zozote ndani ya jumuiya. Mwanachama itamfaa kuawasilisha mawazo yake kwa katibu wa jumuiya wa ngazi husika kwa maandishi.
6. Mwanachama atakopeshwa fedha, gari, nyumba au rasilimali nyingine yoyote iwapo tu ametimiza masharti na vigezo vyote vya jumuiya.
6. Atakuwa mwajiri/mwajiriwa wa taasisi ndogondogo zitakazo azishwa chini ya T.Y.E.C kama vile mabenki ,mashamba viwanda na vitega uchumi vingine.
7. Aweza kuwa mwanachama wa jumuiya zingine ilimradi asivunje katiba.
8. Mwanachama ataweza kukopeshwa fedha aweze kujisomesha na kujiendeleza kielimu ndani na nje ya ya Tanzania ,iwapo tu ameweza kutii vigezo vilivyowekwa na T.Y.E.C.
9. Mwanachama atawezeshwa kujisomesha na kumaliza masomo yake katika ngazi mbalimbali na T.Y.E.C, iwapo tu amekizi masharti ya katiba hii.
10. Mwanachama aweza kuchaguliwa kuiwakilisha jumuiya ndani na nje ya Tanzania kama tu amekidhi masharti ya katiba hii.
11. Mwanachama aweza kupata msaada wakisheria kutoka T.Y.E.C ikiwa ni kwa mambo yake binafsi, iwapo tu amekidhi masharti ya katiba hii.
8
11. WAJIBU WA MWANACHAMA
1. Atashiriki kikamilifu kwenye shughuli zinazohusu jumuiya na taifa kwa ujumla
2. kutoa mwamko wa kielimu ,ushauri na hamasa kwa jamii yake kwa maswala mbalimbali
3. Kuilinda jumuiya zidi ya propaganda za kisiasa zinazoweza kudhoofisha jumuiya na kupunguza ufanisi wake.
4. Kutoa fikra makini, nzuri na mpya zenye makusudi ya kusaidia jumuiya na jamii kusonga mbele.
5. Kwamba kwa vitendo atapinga udhalimu ,unyanyasaji ,uonevu ,ubaguzi na ukandamizaji usio wa msingi ndani ya jamii yake anamoishi.
6. Kwamba yeye na taasisi zingine duniani kote atasimama makini kutetea na kutekeleza haki za binadamu.
7. Kwamba mwana T.Y.E.C atakuwa njia ya kupata majibu ya matatizo mbalimbali yanayoliandama taifa
8. Kuwa mwadilifu na mwaminifu muda wote kwa maswala yanayohusu jumuiya na taifa kwa ujumla wake.
9. Kutoa ushirikiano wa dhati kwa mamlaka husika ilikufanikisha kupatikana na kwa utatuzi wa matatizo au jambo lolote linalohitaji ushirikiano wa mwanachama kwa jinsi ya karibu.
10. Kulipa ada ya kila muhula kwa namna yakufanikisha shughuli za jumuiya.
11. Kwamba mwanachama atapenda ushirikiano na kuunga mkono mambo yote ya jumuiya mara inapo hitajika kufanyika hivyo
12. MWISHO NA UHALI WA KUWA MWANACHAMA
Mtu aweza kuwa mwanachama wa T.Y.E.C kwa wakati wote ambapo ataishi kwa ushirikiano dhabiti pamoja na katiba hii.Lakini pia uhalali wa kufukuzwa /kuondoka katika jumuiya utakuja pale tu
1. Atafukuzwa baada ya kukuika maadili mengine ndani ya jumuiya
9
2. Iwapo tu mwanachama amepoteza uhai wake
3. Ataamua kujiuzulu na kujivua uanachama yeye mwenyewe
4. Mwanachama aliyefukuzwa uanachama ama kujiuzulu uanachama ataweza kurudishwa /kurudi kwenye jumuiya kwa kuandika barua kwa ,katibu wa kata wajumuiya maombi yake yatajadiliwa na kutolewa uamuzi na kamati ya utendaji ya wilaya
5. Aliyejiuzulu uanachama au kufukuzwa atalazimika kurudisha mali za jumuiya au amana alizo nazo kwa maelekezo ya uongozi husika
6. Endapo aliyejiuzulu au kufukuzwa uanachama, pindi arudipo katika jumuiya atalazimika kusajiliwa na atanunua kitambulisho/kadi mpya
SEHEMU YA NNE
UONGOZI WA JUMUIYA
14. VIPIMO VYA KIONGOZI KATIKA JUMUIYA
1. Apende kujishughulisha kiakili, mtafiti na mpelelezi kuhusu mambo ya msingi yenye lengo la kujenga jumuiya.
2. Awe ni mtu wakutafiti matatizo yanayoikumba jumuiya na kutafutia ufumbuzi wa matatizo hayo
3. Awe hodari, makini na mchapakazi wa kuleta mabadiliko kwenye jumuiya na jamii
4. Awe anaaminika , kukubalika mwadilifu na asiwe na historia mbaya katika jamii ikiwa ni pamoja na historia ya uhalifu .
5. Awe ni mzalendo na mwenye uchungu na nchi yake na awe na ushujaa na ushupavu wa kutetea maswala ya msingi yanayogusa wanyonge na maslahi ya taifa.
6. Awe na upeo mpana kiakili na kuwa tayari kujiendeleza kielimu ,na kutumia elimu aliyoipata kwa manufaa ya wengi
7. Awe mkweli kwa maneno na vitendo ,mtetezi na mpenda haki ndani na nje ya Tanzania.
10
8. Kiongozi atathaminiwa zaidi kwa misimamo yake ,asiwe kigeugeu na asiwe mbabaishaji kwa maswala ya jumuiya na katika jamii yake.
9. Awe tayari kukosolewa pale anapoonyesha upungufu na tayari kujisahihisha pindi anapokosolewa.
10. Awe na nidhamu juu ya katiba, viongozi wengine na jamii yake kwa ujumla wake.
11. Apende demokrasia na kuheshimu zaidi, maamuzi ya wengi
12. Aichukie Rushwa kwa vitendo, bila kutishwa na mtu yeyoyote wa taasisi Fulani
15. HAKI ZA KIONGOZI
1. kutoa utetezi na ushahidi kwa kikao chochote kinachomhusu yeye
2. kiongozi aweza kutafuta rufaa kwenye ngazi ya juu ya jumuiya iwapo hataridhika na uamuzi uliomuondoa katika nafasi yake ya awali
3. kiongozi wa T.Y.E.C anazo haki zingine kamazilivyotwajwa kwenye sehemu ya tatu(haki za mwanachama)
4. kiongozi wa jumuiya T.Y.E.C zingine kamazilivyotajwa kwenye sehemu ya tatu ya katiba hii(haki za mwanachama)
16. KUACHIA UONGOZI /KUACHA MADARAKA
1. Muda wa uongozi kumalizika
2. Kama kiongozi amehitaji kujiuzulu ama kuacha nafasi yake
3. Ataacha uongozi kama wale ambao anawaongoza wameishiwa imani nae kuendelea kuwaongoza
4. kama kiongozi amefukuzwa kwa kukiuka katiba ,kanuni na maadili ya uongozi wa jumuiya
5. Iwapo taarifa za kisheria zimeonyesha kiongozi amepatikana na hatia ,kinyume na maadili ya uongozi.
6. Iwapo kiongozi amezoofishwa na maradhi kiasi cha kushindwa kufanya kazi za jumuiya kwa ufanisi
7. Iwapo kiongozi ametutoka duniani (amefariki dunia)
11
SEHEMU YA TANO
VIKAO VYA JUMUIYA/NAMNA MPANGILIO WA VIKAO VYA T.Y.E.C
17. NGAZI YA KATA/SHEHIA
1. Kata itakuwa ndicho kikao na ngazi ya chini kabisa katika jumuiya,na itakuwa vikao vya ngazi ya chini kabisa katika mujukumu ya jumuiya
2. Vikao vya kata vitakuwa na kamati ya utendaji ya kata /shehia
3. Mkutano mkuu wa kata
a. Mwenyekiti wa kata/ shehia wa (T.Y.E.C)
b. Katibu wa kata /shehia
c. Mweka hazina wa kata /shehia
d. Wawakilishi kutoka vitengo vya watoto, wazee,vijana na walemavu wa T.Y.E.C
e. Wenyeviti na makatibu wa idara zote za jumuiya kutoka ngazi ya kata
f. Wajumbe/wawakilishi watano kutoka kata husika
1. MAJUKUMU YA KAMATI YA UTENDAJI KATA/ SHEHIA
a. kujadili maombi ya walio jiuzulu /kufukuzwa uanachama kutaka kurudi jumuiyani na
kisha kuyatolea maamuzi
b. kupokea na kujadili maombi ya wagombea mbalimbali katika nafasi mbalimbali wa kata
c. kuwasilisha majina yawaliopendekezwa kugombea nafasi mbalimbali za uongozi wa kata kupitia katibu wa wilaya
d. kusimamia na kushughulikia kazi za jumuiya kwenye kata/shehia
e. kubuni mbinu pamoja na kusimamia vyanzo mbalimbali vya mapato na miradi ya jumuiya
12
f. kusimamia matumizi,na mwenendo mzima wa fedha za jumuiya kwenye ngazi ya kata
g. kutoa mikakati na mipangilio ya shughuli za maendeleo ya jumuiya katika kata
h. kupima utendaji na ufanisi wa shughuli za maendeleo ya jumuiya kwenye kata /shehia
i. kusikiliza na kutoa maamuzi ya rufani za wanachama waliofukuzwa au kujiuzulu kutoka jumuiyani
j. kubuni mikakati mipya na mbinu za kuleta mafanikio kwa ufanisi mkubwa
k. kutoa mapendekezo ,na misimamo ya jumuiya kwa ngazi ya kata kwa niaba ya ngazi za juu
l. kutathmini na kupitisha bajeti ya kata/shehia
m. kupokea ,kujadili na kupitisha taarifa ya fedha ya kata ya kila muhula
n. itakutana walau mara nne kila muhula
2. WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA KATA
a. Mwenyekiti wa kata wa jumuiya
b. Katibu wa jumuiya
c. Mweka hazina wa jumuiya
d. Wenyeviti ,makatibu na makatibu wa idara na vitengo vya jumuiya ngazi ya kata
e. Wajumbe kumi waliowanachama wa T.Y.E.C ngazi ya kata/shehia
3. KAZI ZA MKUTANO MKUU NGAZI YA KATA
a. Kupima mwenendo wa shughuli za kila siku za jumuiya ngazi ya kata.
b. Kutathmini maendeleo ya kata kwa ujumla wake.
c. Kuweka baraka maamuzi yote yaliyo amuliwa kupitia ngazi za chini ya jumuiya.
13
d. Kutoa mapendekezo ya muhimu yanayohitaji kupelekwa kwenye mijadala ya vikao vya juu ya jumuiya.
e. Kuidhinisha kanuni/taratibu mpya zilizo tungwa kwa ajili yakufanisi shughuli za jumuiya ngazi ya kata, kabla ya kuwasilishwa kwa maandishi kwenda ngazi za juu za jumuiya.
4. KAZI ZA MWENYEKITI WA KATA/SHEHIA
a. Yeye ndiye msimamizi mkuu wa shughuli za kila mara ngazi ya kata
b. Ndiye msemaji na mhamasishaji mkuu katika kata/shehia
c. Ndiye mwenyekiti wa vikao na mikutano mbalimbali kwenye kata/shehia
d. Ataongoza shughuli zote za uzalishaji katika kata/shehia
e. Atashiriki kikamilifu kwenye kutoa ufumbuzi na majibu ya migogoro mbalimbali inayoibuka kwenye jumuiya.
5. KAZI ZA KATIBU WA KATA /SHEHIHA
a. Ndiye mtendaji mkuu wa jumuiya kwenye ngazi ya kata/shehia.
b. Kutunza takwimu ya wanachama, na taarifa zingine zinazohusu wanachama kwa ngazi ya kata/shehia.
c. Kuwa na kumbukumbu sahihi juu ya mali zote za jumuiya zilizoko kwenye mamlaka ya kata.
d. Ndiye mdhibiti na msimamizi mkuu wa mali za jumuiya kwenye nagazi ya kata.
e. Atawajibika juu ya upotevu wa nyaraka na taarifa za kila siku za jumuiya kwa ngazi ya kata/shehia kwa namna itakavyo elekezwa
f. Atawajibika juu ya upotevu wa nyaraka na taarifa zingine za jumuiya kwa uzembe au makusudi kwa ngazi ya kata/shehia
g. kufanya kazi nyingine yoyote itakayo kuwa imetajwa penginepo kwenye katiba hii
6. KAZI ZA MWEKA HAZINA WA KATA/SHEHIA
a. Ndiye msimamizi wa fedha na taarifa zingine za fedha kwenye kata/shehia.
b. Ndiye atakuwa mdhibiti wa taarifa za fedha kwenye kata/shehia.
14
c. Kubuni na kutafuti fedha kwa ajili ya maendeleo ya jumuiya.
d. Kuweka kumbukumbu sahihi za mapato na matumizi ya fedha
e. Kutengeneza na kuwasilisha bajeti ya jumuiya kwa ngazi ya kata/shehia
f. Kutoa taarifa ya mapato na matumizi ya fedha kwa ngazi ya kata
18. NGAZI YA WILAYA
1. Wilaya itakuwa na vikao kama ifuatavyo
a. Kamati ya utendaji ya wilaya
b. Mkutano mkuu wa wilaya
1. WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA WILAYA
a. Mwenyekiti wa wilaya wa jumuiya
b. Katibu wa wilaya wa jumuiya
c. Mweka hazina wa wilaya wa jumuiya
d. Wenyeviti, makatibu wa kata zote zilizoko kwenye wilaya husika
e. Wenyeviti, makatibu wa idara na vitengo mbali mbalimbali katika wilaya
f. wenyeviti na makatibu wa idara na vitengo mbali mbali ngazi ya wilaya
g. wawakilishi kumi kutoka kata tano zilizo karibu
2. KAZI ZA MKUTANO MKUU WA WILAYA
a. kupima mwenendo wa shughuli za jumuiya kwenye wilaya
b. kutathmini maendeleo ya wilaya
c. kutoa mikakati na miongozo kwa maendeleo ya wilaya
d. kutoa maamuzi yahusuyo jumuiya kwa ngazi ya kata ,kwa mambo yote yaliyo onekana kutokupata majibu kwenye vikao vya chini vya jumuiya
15
e. kupitia na kuidhinisha sheria na taratibu mpya zilizo tungwa kwa maendeleo na ufanisi wa jumuiya kabla ya kupelekwa kwenda ngazi zingine za jumuiya
f. itakutana walau mara mbili kila muhula
3. KAZI ZA WAJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI YA WILAYA
a. Mwenyekiti wa wilaya wa jumuiya
b. katibu wa wilaya wa jumuiya
c. Mweka hazina wa wilaya wajumuiya
d. Wenyeviti na makatibu wa idara mbalimbali ngazi ya wilaya
e. Wenyeviti na makatibu wa vitengo mbalimbali ngazi ya wilaya
f. makatibu na wenyeviti wa kata tano za karibu
g. makatibu na wenyeviti wa idara na vitengo kutoka kata tano zilizo karibu
h. wawakilishi kumi kutoka kata tano zilizo karibu
4. KAZI ZA KAMATI YA UTENDAJI YA WILAYA
a. Kusimamia na kutoa mwenendo wa shughuli za jumuiya wilayani
b. Kutekeleza shughuli za jumuiya kwenye wilaya
c. Kupitisha majina ya wagombea ,wanafasi malimbali kwenye wilaya kutoka kata zililizopo kwenye wilaya
d. Kutathmini maendeleo ya jumuiya kwenye wilaya na kutoa misimamo wa shughuli za jumuiya kwenye wilaya hiyo
e. Kubuni mikakati ya kuhamasisha watu kwa shabaha ya kufanikisha malengo yenye kuzaa matunda.
f. Kutuma majina ya wagombea wa nafasi mbalimbali ngazi ya wilaya kwenda mkoani.
g. Kushirikiana na kamati ya utendaji za kata kutoa maamuzi ya wanaojiuzulu au kufukuzwa na wanaoomba tena kurudi jumuiyani.
16
h. Kujadili na kupitisha rufaa ya walalamikaji waombaji ngazi za chini.
i. Kuwaondoa madarakani viongozi ngazi ya kata waliokiuka taratibu, kanuni na katiba ya jumuiya.
j. Kupokea na kupitisha taarifa ya kila muhula kuanzia kata hadi kata.
k. Kujadili na kupitisha bajeti ya jumuiya ngazi ya wilaya na kupitia bajeti ngazi ya kata.
l. Kuwajibika na kutuma wilayani taarifa za maendeleo ya jumuiya ya kila mwezi na kwa wakati wowote itakapobidi kufanya hivyo.
m. Kufanya kazi nyingine yoyote ile itakayo kuwa imetajwa penginepo kwenye katiba hii.
n. Itakutana walau mara tatu kila muhula
5. KAZI ZA MWENYEKITI WA WILAYA
a. Atakuwa msimazi wa shughuli za jumuiya kila siku kwenye wilaya.
b. Atakuwa msemaji mkuu wa maswala yanayohusu jumuiya kwenye wilaya.
c. Atakuwa kiongozi wa shughuli na vikao vyote katika wilaya.
d. Aweza kuitisha kikao cha dharura ,baada ya kufanya mawasiliano na katibu wa wilaya.
e. Aweza kufanya kazi yoyote ile itakayokuwa imetajwa kwenye katiba hii.
6. KAZI ZA KATIBU WA WILAYA
a. Ndiye mtendaji mkuu wa jumuiya ngazi ya wilayani.
b. Atatunza taarifa za jumuiya ikiwa ni pamoja na taarifa za rasilimali za jumuiya wilayani.
c. Ndiye mdhibiti mkuu wa mali za jumuiya katika wilaya.
d. Atawajibika kutoa taarifa za kila siku kuhusu maendeleo ya jumuiya kwenda ngazi za juu wilayani
e. Atafanya kazi nyingine yeyote itakayokuwa imetajwa penginepo kwenye katiba hii
7. KAZI ZA MWEKA HAZINA WA WILAYA
a. kubuni na kutafuta fedha kwa ajili ya shughuli za jumuiya wilayani
17
b. kuweka kumbukumbu za mapato na matumizi ya jumuiya wilayani
c. kuandaa bajeti ya jumuiya ngazi ya wilaya
d. ndiye mdhibiti na mhusika wa maswala yote yahusuyo fedha katika jumuiya ngazi ya wilaya
e. aweza kufanya kazi nyingine yoyote ile iliyotajwa kwenye katiba hii
19. NGAZI YA MKOA
Mkoa utakuwa na vikao vifuatavyo:
a. Mkutano mkuu wa mkoa.
b. Kamati ya utendaji ya mkoa.
1. WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA MKOA;
a. Mwenyekiti wa Jumuiya mkoa
b. Katibu wa Jumuiya mkoa
c. Mweka hazina wa jumuiya mkoa.
d. wenyeviti na makatibu wa Wilaya pamoja na kata
e. Wenyeviti na makatibu wa mkoa wa idara na vitengo .
f. Wawakilishi (10) Toka wilaya zilizo karibu.
2. MAJUKUMU YA MKUTANO MKUU WA MKOA.
a. Kupima na kuona utekelezaji wa shughuli za jumuiya za kila siku mkoani.
b. Mkutano mkuu utatoa tathmini ya mkoa kila pindi wakutanapo.
c. Itashughulika kutoa miongozo na mwelekeo / maendeleo ya mkoa.
d. Mkutano mkuu wa mkoa utakutana mara ( tatu) kila baada ya miezi mitatu.
3. KAMATI YA UTENDAJI YA MKOA HUUNDWA NA WAJUMBE WAFUATAO.
a. Mwenyekiti wa mkoa
b. Katibu wa mkoa
c. Mweka hazina mkoa
d. Wenye viti na makatibu wa Idara na vitengo mbalimbali za mkoa,
18
e. Wenyekiti na makatibu wa wilaya na kata katika mkoa huo
f. Wajumbe (10) kutoka wilaya (5) zilizo karibu.
4. KAZI ZA KAMATI YA UTENDAJI YA MKOA
a. Kusimamia shughuli na utendaji wa Jumuiya katika mkoa huo
b. Kutekeleza maagizo na mikakati ya Jumuiya kutoka ngazi za juu ya Jumuiya.
c. Kubuni na kusimamia vyanzo vya mapato ya Jumuiya katika mkoa huo.
d. Kutathimini maendeleo ya jumuiya katika mkoa huo
e. Kubuni mbinu na mikakati mipya ya kuendeleza Jumuiya katika mkoa
f. Kutoa maamuzi na muafaka kwa wanachama waliojiuzulu na kufukuzwa na kuomba upya kujiunga na Jumuiya.
g. Kupokea kujadilili na kupitisha majina ya wagombea nafasi mbali mbali ngazi ya (wilaya) pia na kata
h. Kuwachukulia hatua za kinidhamu viongozi ngazi wilaya wakishirikiana na kamati ya utendaji ya mkoa
i. Itapokea rufaa na mapendekezo toka ngazi ya wilaya.
j. Kufanya maandalizi ya mkutano mkuu wa mkoa
k. Itawajibika na kutuma taarifa za maendeleo ya Jumuiya kwa ngazi za juu kila mwezi
l. Itajadili na kupitisha bajeti ya Jumuiya kwa ngazi ya (Mkoa).
m. Itapokea kusajili na kupitisha taarifa ya Idara na vi tengo mbalimbali kwa kila muhula.
n. Kujihusisha na kazi nyingine yoyote ambayo itakuwa imetajwa katika katiba hii
o. Itakutana mara (3) kila baada ya miezi mitatu.
5. KAZI ZA MWENYEKITI WA MKOA
a. Ndiye msimamizi wa shughuli za kila siku za Jumuiya katika mkoa
b. Atakuwa msemaji na mhamasishaji mkuu wa Jumuiya mkoani
c. Kuongoza mikutano yote ya Mkoa na pindi inapobidi
d. Atafanya kazi yoyote iliyotajwa penginepo kwenye katiba hii
6. KAZI ZA KATIBU WA MKOA
a. Atakuwa ndiye mtendaji mkuu wa Jumuiya katika mkoa.
19
b. Kutunza orodha yote ya wanachama na taarifa zingine zote zinazo wahusu wanachama wa jumuiya
c. Atawajibika kutunza kumbukumbu zote na mali za jumuiya kwa ngazi hiyo
d. Ndiye atakuwa mdhibiti na msimamizi mkuu wa rasilimali zote za Jumuiya katika mkoa.
e. Atahusika akishirikiana na kamati ya utendaji kutoa taarifa za kila mwezi ngazi ya mkoa kwa ngazi za juu.
f. Aweza kufanya kazi nyingine yeyote ambayo itakuwa imetajwa katika katiba hii.
7. KAZI ZA MWEKA HAZINA WA MKOA.
a. Kwamba yeye akishirikiana na uongozi wengine watatafuta fedha kwa ajili ya Jumuiya.
b. Atawajibika kuweka kumbukumbu zote za mapato na matumizi kwa Jumuiya mkoani
c. Atawajibika kuandaa bajeti ya jumuiya ngazi ya mkoa
d. Kutoa taarifa ya mapato na matumizi ya jumuiya mkoa
20. NGAZI YA TAIFA
Jumuiya itakuwa na vikao vya namna tofauti kama ifuatavyo.
a. Mkutano mkuu wa Taifa
b. Kamati kuu ya Taifa
1. WAJUMBE WATAKAO WAKILISHA KWENYE MKUTANO MKUU WA TAIFA.
a. Mwenyekiti / Rais wa jumuiya ngazi ya Taifa
b. Makamu mwenye kiti wa Taifa (Bara)
c. Makamu mwenyekiti Taifa (Zanzibar)
d. Katibu mkuu
e. Naibu katibu mkuu Bara
f. Naibu katibu mkuu (Zanzibar)
g. Mweka hazina Taifa
h. Wajumbe wa baraza la wadhamini wa jumuiya.
i. Wajumbe wa kamati kuu Taifa.
j. Wenyeviti na makatibu wa jumuiya wa mikoa
20
k. Wenye viti na makatibu wa Idara mabalimbali za Jumuiya Taifa , .
l. Wenyeviti na makatibu wa vitengo vya Jumuiya Taifa.
2. KAZI ZA MKUTANO KUU WA TAIFA.
a. Kutoa mapendekezo yahusuyo katiba na ikibidi kufanya marekebisho ya lazima
b. Itatoa maelekezo juu ya utekelezaji wa itikadi na malengo ya Jumuiya
c. Itatoa maamuzi ya mwisho yahusuyo jumuiya penginepo kutajwa katika katiba hii
d. Kupima na kufanya tathmini ya shughuli za Jumuiya katika ngazi mbalimbali
e. Mkutano mkuu wa Taifa utafanyika walau mara 3 kila muhula
3. WAJUMBE WA KAMATI KUU TAIFA.
a. Rais / Mwenyekiti wa Jumuiya Taifa.
b. Makamu mwenyekiti wa Taifa (Bara)
c. Katibu mkuu tai fa
d. Naibu katibu mkuu (Bara )
e. Naibu katibu mkuu (Zanzibar)
f. Mwenyekiti na katibu wa Baraza la wadhamini la Jumuiya.
g. Mweka hazina Taifa
h. Wajumbe (20) kumi kutoka bara na (10) zanzibar
i. Wenye viti na makatibu Taifa wa Idara na vitengo kutoka zanzibar
j. Wenyeviti na makatibu wa vitengo vya Jumuiya (Taifa)
k. Wenyeviti makatibu wa Jumuiya mikoa na wilaya
4. KAZI ZA KAMATI KUU YA TAIFA (JUMUIYA)
a. Kujadilili maombi ya wagombea nafasi mbalimbali Taifa na mikoa
b. Kutoa maamuzi ya mwisho yahusuyo rufaa kwa waliojiuzulu (au) kufukuzwa ngazi ya Taifa na mikoa wakishirikiana na kamati za utendaji za mikoa hiyo.
c. Itawajibika kufanya na kupanga ratiba na mikakati mengineyo yahusuyo maendeleyo ya Jumuiya Taifa
21
d. Kuandaa sera mikakati yahusuyo vitengo na idara mbalimbali na jamii na mwisho kuwasilisha kwenye mkutano mkuu wa Taifa kwa mujibu wa vikao vyake
e. Kufuatilia utendaji wa kila mkoa na utekelezaji wa shughuli na sera za jumuiya katika mikoa .
f. Kutathimini utekelezaji wa shughuli zote za jumuiya nchini
g. Kupokea kujadili na kupitisha taarifa ya kila idara na vitengo v ya Jumuiya
h. Kuweka kanuni na utaratibu kuhusu vifaa, fedha, uajiri, uchaguzi, vitengo, nidhamu na kuweka katika taratibu za jumuiya.
i. Kupokea na kupitisha taarifa na kazi za Baraza la wadhamini la jumuiya kila muhula
j. Kupanga na kupitisha ada na viingilio vya wanachama katika Jumuiya.
k. Itahusika kwenye kutoa mapendekezo na marekebisho ya katiba na sera zingine za Jumuiya kwa mkutano mkuu wa Jumuiya
l. Kufuatilia utendaji wa mkoa hadi mkoa
m. Kufukuza (au) kuvua uanachama. Mwanachama/ kiongozi yoyote ngazi ya mkoa na Taifa.
n. Kujadili na kupitiha bajeti ya Jumuiya
o. Kamati kuu ya Jumuiya itakutana na mara tatu(3) kwa kila muhula.
21. KAMATI KUU MAALUMU (ZANZIBAR)
(a) Hii itatambuliwa kama sehemu ya kamati kuu ya Taifa.
(b) Shughuli zote zitafanywa kwa maelekezo ya (kamati kuu ya Taifa)
(c) Itabidi iwajibike pale inapobidi kwa kamati kuu Taifa.
(d) Shughuli zake zote zitafanyika upande wa Tanzania Zanzibar isipokuwa kwa maelekezo yatakayotolewa na kamati kuu Taifa
(e) Makamu mwenyekiti Zanzibar na Naibu katibu mkuu kutoka Zanzibar watakuwa viongozi wawili wakuu wa vikao vya upande wa Zanzibar.
1.WAJUMBE WA KAMATI MAALUMU YA (KAMATI KUU TAIFA)
(a) Makamu mwenyekiti Taifa (Zanzibar).
(b) Naibu katibu mkuu Taifa Zanzibar
(c) Wajumbe wa kamati kuu Taifa toka Zanzibar.
(d) Wenyeviti na makatibu wa vitengo na idara za jumuiya toka Zanzibar.
22
2. KAZI ZA KAMATI MAALUMU YA KAMATI KUU YA TAIFA.
(a) Kupanga shughuli zote zihusiyo jumuiya Zanzibar.
(b) Kutekeleza shughuli na maagizo ya jumuiya kama ilivyo ekelezwa na kamati kuu ya Taifa.
(c) Kuweka ufuatiliaji makini na sahihi, kwa kila mkoa wa Zanzibar kabla ya kuwasilisha taarifa yake kwa kamati kuu.
(d) Kutathmini utekelezaji wa shughuli zote za jumuiya katika Zanzibar.
(e) Kujadili na kutolea maamuzi rufaa za walojiuzulu / kufukuzwa kwa mkoa na Taifa kwa upande wa Zanzibar.
(f) Kujadili na kupitia bajeti ya ofisi ndogo ya jumuiya (Zanzibar)
(g) Itafanya jukumu lingine lolote kwa maagizo ya kamati kuu ya Taifa.
(h) Itakutana walau mara (3) kila mhula.
SEHEMU YA SITA
22. SEKRETARIETI YA JUMUIYA
(1) Jumuiya itakuwa na sekretarieti ya jumuiya katika kila ngazi ya jumuiya. (Taifa,Mkoa, Wilaya na Kata)
(2) Katika ngazi kuu/Taifa kutakuwa na sekretarieti makao makuu ya jumuiya JIJINI (ARUSHA) Na katika ofisi ndogo ya jumuiya kule MJINI (ZANZIBAR)
(3) Sekretarieti ya kila ngazi itakuwa
(a) IDARA YA HABARI, UTAMADUNI NA MICHEZO
(b) IDARA YA ULINZI NA USALAMA
(c) IDARA YA MAMBO YA NJE NA UHUSIANO WA JUMUIYA
(d) IDARA YA MAMBO YA NDANI NA UHUSIANO WA JUMUIYA
(e) IDARA YA UCHAGUZI NA USIMAMIZI
(f) IDARA UCHUMI TAKWIMU, NA MIPANGO.
(g) IDARA YA GEOGRAPHIA NA MAJANGA.
(h) IDARA YA AFYA NA MAENDELEO
(i) IDARA YA VIWANDA NA UCHUMI,
(j) IDARA YA ELIMU
(k) IDARA YA SAYANSI NA TEKNOLOGIA
23
(l) IDARA YA MADINI NA NISHATI
(m) IDARA YA UWEZESHAJI NA UJASIRIAMALI
(n) IDARA YA KILIMO, UMWAGILIAJI NA MAZINGIRA.
(o) IDARA YA CHAKULA
(p) IDARA YA MIFUGO
(4) Idara zitafanya kazi na shughuli za (Jumuiya) za utendaji za kila siku.
(5) Sekretarieti ya ngazi husika itaundwa mara baada ya wajumbe wa kikao cha utendaji kuundwa.
(6) Mara baada ya majina ya wakuu wa idara kupendekezwa na katibu wa jumuiya kamati ya utendaji itakubali au kukataa majina hayo na pindi wapendekezwapo watakuwa ndio wajumbe wa sekretarieti ya jumuiya ya ngazi husika.
(7) Katibu wa jumuiya ndiye kiongozi wa sekretarieti ya ngazi husika. Na kwamba yeye na viongozi wa jumuiya wengine kwa ngazi husika wataweza kuondolewa kwenye nafasi zao na hata uanachama
(8) Kwa yeye naibu katibu mkuu (Zanzibar) atakuwa katibu wa vikao vyote vya sekretarieti ya jumuiya ya kamati kuu ngazi ya Taifa
(9) Kwa mikoa, wilaya na kata watachagua makatibu wao baada ya kuundwa.
(10) Mweka hazina naye akiwa ni mjumbe wa sekretarieti wa ngazi yake.
(11) Itakutana walau mara (6) kila muhula.
23.SEKRETARIETI YA JUMUIYAYA KAMATI MAALUM YA KAMATI KUU YA TAIFA.
Kutakuwa na sekretariati ya jumuiya ya kamati maalum ya kamati kuu ya Taifa.
1. Kamati kuu maalum itakuwa na idara kama ilivyo tajwa kwenye katiba hii / Idara za jumuiya
2. Itafanya shughuli za Jumuiya za kila siku kwa niaba ya kamati kuu Taifa. Upande wa zanzibar
3. Naibu katibu mkuu ( Zanzibar) atakuwa kiongozi wa sekretariati.
4. Katibu wa sekretariti ya kamati maalum ya kamati kuu ya Taifa atachaguliwa mara baada ya sekretariti kuundwa.
24
SEHEMU YA SABA
24. VITENGO VYA JUMUIYA.
1. Jumuiya itakuwa pia na Vitengo vifuatavyo
a. Wazee
b. Walemavu.
c. Watoto.
2. Vitengo vyote vya Jumuiya vitakuwa chini ya uongozi wa ngazi husika na vitawajibika kwa ngazi hiyo kupitia kwa katibu wa (Jumuiya wa ngazi hiyo.
3. Ikibidi kila kitengo kitatunga taratibu na sheria za kusimamia shughuli zake. Kanuni na sheria zitakazotungwa lazima zipitiwe na kupewa idhini na kamati kuu ya Taifa.
d. Wenyeviti wa vitengo na makatibu watapendekezwa na uongozi wa Jumuiya kwa ngazi husika na baadae kupitishwa na kamati ya utendaji kwa ngazi ya kata, wilaya na mkoa na kamati kuu kwa Taifa
f. Kila kitengo kitatoa taarifa ya maendeleo kwa kamati kuu kila muhula.
SEHEMU YA NANE
25. BARAZA LA WADHAMIANI LA JUMUIYA .
1.Wajumbe wa baraza la wadhani la jumuiya ni
a.Mwenyekiti wa baraza la wadhamini la jumuiya
b.katibu wa baraza la wadhamini la jumuiya
c.wajumbe wengine kumi walio wanachama halisi wa T.Y.E.C
2.Madaraka na mamlaka ya baraza la wadhamini ni kama,
a.baraza la wadhamini litakuwa na madaraka na mamlaka yake kama iliavyo elekezwa kwenye sheria ya wadhamini.
25
b.kazi na majukumu ya baraza la wadhamini itakuwa sambamba na maelekezo ya kila siku ya `kamati kuu ya taifa
c. Mdhamini atahudumu na kusimamia majukumu yake ya kila siku kwa kipindi cha miaka mitano .vilevile mdhamini aweza kuchaguliwa/kuteuliwa kuishika nafasi hiyo kwa kipindi kingine cha miaka miatano.
d. Kwa nafasi yake mweka hazina wa taifa atakuwa katibu wa baraza la wadhamini la jumuiya.
e. Baraza la wadhamini la jumuiya litakutana kufanya vikao vyake walau mara nne kila muhula 3.Mdhamini aweza kusimamishwa, kupumzishwa,au kufukuzwa katika udhamini kwa mamlaka ya kamati kuu ya taifa.
a. ikiwa afya ya mdhamini ni mbaya kiasi cha kushindwa kutekeleza majukumu yake ya kila siku ya udhamini
b. Ikiwa uwezo wake wa kufanikisha shuguli zake za kila siku umepungua/uwezo kupungua
c. Ikiwa ameishi nje ya taifa la Tanzania kwa muda wa mwaka mmoja mfululizo.
d. ikiwa mdhamini amekwenda kinyume na katiba ya jumuiya
e. ikiwa kamati kuu ya taifa imemkuta mdhamini na kosa ambalo halikustahili kufanywa na mdhamini.
f. ikiwa mdhamini amefilisiwa na akashindwa kujikomboa katika kipindi cha miezi mitano ya udhamini wake.
4. Ikiwa mdamini anajiuzulu, kufariki au kusimamishwa udhamini utaratibu wa kawaida kama ilivyo elekezwa katika katiba hii kutumika ili kujaza nafasi iliyoachwa wazi
5. Ikiwa mdhamini anajiuzulu barua ya kujiuzulu itatumwa kwa kamati kuu ya taifa kupitia kwa mwenyekiti wajumuiya..
6. Vilevile wajumbe wa baraza la wadhamini wanaweza kumchagua mwenyekiti wamuda kuongoza kikao cha siku hiyo ikiwa mwenyekiti wa baraza la wadhamini hayupo kikaoni.
7. Majukumu na kazi za baraza la wazamini la jumuiya.
26
a. Itasimamia kwa sheria mali zote za jumuiya ikiwa ni mali za kuondesheka na zisizoondosheka
b. Baraza laweza kufanya kazi yoyote yenye kulenga kuimarisha jumuiya,kwa marejeo ya madhumuni na malengo ya jumuiya.
c. Baraza la wadhamini lina mamlaka ya kuunda kamati na idara ndogondogo kwa madhumuni ya kurahisha majukumu yake ya kila siku
d. Kutoa taarifa ya kiutendaji ya kila siku kwa kwa kamati kuu kwa kila muhula
e. Kwa umakini ya bila kwenda kinyume na sheria ya wadhamini baraza laweza kuitisha kikao cha dharura kwa lengo la kufanikisha shughuli zake.
SEHEMU YA TISA
26. VIONGOZI WAKUU WA JUMUIYA NA NAFASI ZAO KATIKA JUMUIYA
Viongozi watakao tambulika kama viongozi wakuu wa jumuiya na nafasi zao watakuwa kama ifuatavyo.
a. Mwenyekiti /Rais wa Jumuiya Taifa.
b. Makamu wa mwenyekiti wa Taifa (Bara)
c. Makamu wa Mwenyekiti wa Rais (Zanzibar)
d. Katibu mkuu
c. Naibu katibu mkuu (Zanzibar)
f. Naibu katibu mkuu (Zanzibar)
g. Mweka hazina wa Taifa
1. MWENYEKITI /RAIS WA JUMUIYA TAIFA.
a. Atakuwa msemaji na mhamasishaji.mkuu wa jumuiya
b. Atakuwa mwenyekiti wa mkutano mkuu wa Taifa na kamati kuu wa Taifa.
27
c. Mwenyekiti /Rais atakuwa na uwezo wa kuteua wajumbe wa kamati kuu baada ya kuhojiana na katibu mkuu.
d. Aweza pia kutengua Ujumbe wa yule yoyote aliye chaguliwa kwa mawasiliano na katibu mkuu.
e. Iwapo kwa sababu zozote zile mwenyekiti /Rais hayupo kikazi au kwa vinginevyo makamu mwenyekiti (Zanzibar) atakaimu nafasi yake na makamu mwenyekiti bara atakuwa makamu mwenyekiti /Rais kwa wakati huo.
f. Na iwapo kiti cha Rais/ mwenyekiti na jumuiya kimeachwa wazi kwa sababu za kujiuzulu au kufariki au (utaratibu) ulizoelewa hapo waweza kufuatwa kabla ya kamati kuu ya Taifa kutangaza kiti kuwa wazi na kufanyiwa taratibu za uchaguzi.
g. Ataweza kuondolewa madarakani kwa kura ya kutokuwa na imani kwa theluthi mbili ya kura halali zilizopigwa na wajumbe waliohudhuria kikao hicho.
2. MAKAMU WENYEVITI TAIFA
a. Makamu mwenyekiti wa (Bara) atawajibika kumsaidia Rais / Mwenyekiti upande wa bara, hali kadhalika makamu mwenyekiti (Zanzibar) atafanya kazi zaidi upande wa (Zanzibar).
b. Watashirikiana na Rais/ mwenyekiti kwa karibu
c. Wataweza pia kuondolewa madarakani kwa kura ya kutokuwa na imani zaidi ya nusu ya kura zote halali zilizopigwa kwa wajumbe walio hudhuria kikao hicho.
d. Majukumu na mipaka itategemea zaidi maagizo ya Rais / Mwenyekiti wa Taifa.
3. KATIBU MKUU.
a. Huyu ndiye mtendaji mkuu wa jumuiya
b. Atakuwa ni katibu wa vikao vya mkutano mkuu wa Taifa na kamati kuu ya Taifa.
c. Atakuwa na uwezo wa kuajiri,kuteua, kufukuza na kusimamia nidhamu ya waajiriwa kwa mujibu wa katiba hii na sheria za jamuhuri ya muuungano wa Tanzania.
d. Aweza kujihusisha na kazi nyingine yoyote itakayokuwa imetajwa penginepo katika ratiba hii
28
4. NAIBU MAKATIBU WAKUU.
a) Mmojawapo kati ya Naibu katibu mkuu (Zanzibar au kutoka (bara ) ataweza kukaimu nafasi ya katibu mkuu wakati hayupo.
b) Naibu katibu mkuu kutoka Zanzibar atajikita zaidi upande wa Zanzibar na Naibu katibu mkuu (Bara) atajikita (zaidi ) Tanzania (Bara)
c) Watafanya shughuli zao nyingi chini ya maelekezo ya katibu mkuu wa Jumuiya.
d) Wataweza kufanya kazi nyingine yoyote itakayo kuwa imetajwa katika katiba hii.
5. MWEKA HAZINA TAIFA.
a) Mweka hazina itampasa kuwa ndiye katibu wa baraza la wadhamini.
b) Atadhibiti mapato na matumizi ya fedha za Jumuiya.
c) Kwamba yeye kwa kushirikiana na viongozi wachache wenye taaluma ya (Uchumi) wataunda Bajeti ya Jumuiya.
SURA YA KUMI
MAMBO MENGINE YAHUSUYO JUMUIYA.
27. UCHAGUZI.
1. Uchaguzi mkuu wa uongozi wa (Jumuiya) utafanyika kila baada ya miaka (mitano) na vinginevyo kwa maelekezo ya kamati kuu ya Taifa.
2. Kwa kila uchaguzi kila ngazi ya jumuiya itasimamiwa na ngazi iliyoko juu na kwa taifa itatolewa maelekezo na kamati kuu ya taifa
3. Iwapo nafasi yoyote ya uongozi itaachwa wazi na kiongozi uchaguzi mwingine utaitishwa bila kusubiri muda wa miaka mitano kutimu.
4. Uchaguzi wa jumuiya utafanywa kwa nidhamu na usiri.
28. AKIDI ZA VIKAO.
Ili kukidhi nidhamu ya demokrasia Akidi ya kikao lazima iwe ni nusu ya wajumbe wote waliopaswa kuhudhuria kwenye kikao hicho.
29
29. UITISHAJI WA VIKAO VYA JUMUI YA.
1. Katibu wa jumuiya ndiye ataitisha vikao vyote vya jumuiya mara tu baada ya kushauriana na mwenyekiti wake
2. Vikao na mikutano mikuu ya Taifa na mikoa vitaitishwa kwa taarifa isiozidi wala kupungua siku (14)
3. Kwa mikutano inayohusu kamati ya utendaji ya wilaya na kata vitaitishwa kwa taarifa ya siku kumi.(10)
4. Katika hali isiyo ya kawaida vikao na utaratibu ulioelezwa kwa ibara ndogo ndogo za (2) na (3) ya sehemu hii yaweza kuwa kinyume kutegemea udharura wa tukio au kikao.
30. MJUMBE AWEZA KUPOTEZA UJUMBE KAMA.
Kama mjumbe ambaye hata hudhuria vikao vinane mfululizo bila taarifa inayo kubalika aweza kupoteza sifa na atakuwa ajivua ujumbe moja kwa moja.
31. RATIBA ZA VIKAO
Kila kikao cha jumuiya kitafanyika kwa muda uliotajwa katika katiba hii isipokuwa ikitokea jambo la dharura au muhimu kulazimu kutofanyika kwa kikao.
32. ANAYE KAIMU MADARAKA
1. Kama kiongozi au Mjumbe kwa sababu yoyote ile hawezi kutekeleza kazi zake kwa muda au amesimamishwa kwa mujibu wa katiba au kwa kanuni na taratibu zingine za Jumuiya.
2. Kwa mamlaka ya uongozi wenye mamlaka ya kutoa kiongozi au mwanachama yeyote kukaimu nafasi hiyo. Isipokuwa tu awe na sifa na uwezo wakukaimu nafasi hiyo.
3. Muda wa kukaimu utakwisha pindi tu anayekaimiwa kurudi madarakani (au mwanachama kurudi madarakani (au mwanachama mwingine kuteuliwa kushika nafasi. Hiyo na vilevile aliye kaimiwa 4.Anatakiwa kurudi nafasini kabla ya miezi (3) kabla ya nafasi hiyo kujazwa na mtu mwingine) kwa mujibu wa masharti ya katiba hii. Isipokuwa pale kamati kuu itakapo kuwa imelekeza vinginevyo.
33. KURA ZENYE KUHITAJI UAMUZI
Maamuzi ya mwisho yatafikiwa pale kama jambo limeungwa mkono kwa Takribani nusu ya wanachama wote walioshirikiana kupiga kura hizo za maamuzi, isipokuwa pale ilipoelekezwa. Tofauti na katiba hii.
30
34. KAMATI YA NIDHAMU NA USULUHISHO.
Kwa maelekezo ya kamati kuu ya Taifa, chombo chenye wajumbe wasiopungua (kumi na mbili) kitaundwa kwa kila (ngazi) kuanzia (kata) hadi (Taifa). Itakayo husika kunidhamu na kutoa usuluhishi. Chombo cha nidhamu kitahusika kwa nidhamu na kusuluhisha wanachama na viongozi wa Jumuiya isipokuwa vinginevyo ilivyo elekezwa kwenye katibu hii. Ila tu kwa vile itakapo elekezwa vinginevyo kwenye katiba hii
35. VITENGO NA TAASISI ZA JUMUIYA.
Kamati kuu ya Taifa itakuwa na majukumu ya kulinda taasisi, vitengo, vitakavyoendeshwa na kusimamiwa na Jumuiya na malengo na maendeleo ya jumuiya Taasisi hizo zitajitungia taratibu zao na kujiendesha zenyewe vilevile kamati kuu yaweza kuzivunja pale inapobidi kufanya hivyo.
Hivyo hivyo pasipo kuathiri masharti ya katiba hii Jumuiya yaweza kutoa upendeleo kwa mtu yoyote, Jumuiya, Taasisi, Jamii, au kikundi chochote kwa shabaha ya kufanikisha sera na itikadi ya jumuiya husika.
36. MABADILIKO /MAREKEBISHO YA KATIBA HII.
1) Katiba hii yaweza kufanyiwa marekebisho au mabadiliko na kamati kuu ya Taifa (kwa kushirikiana na mkutano mkuu wa Taifa.
2) Iwapo katiba hii itafanyiwa marekebisho ni vyema kuhudhuriwa na akidi ya wajumbe wasiopungua theludhi mbili ya wote walio takiwa kuhudhuria.
37. JUMUIYA KUINGIA MSETO NA ASASI ZINGINE.
1. Jumuiya yaweza kuunga mkono mapendekezo ya kujiunga na asasi zingine, iwapo tu itaungwa mkono na theluthi mbili ya wajumbe wa mkutano mkuu wa Taifa ya waliohudhuria.
2. Mapendekezo ya kuungana na asasi zingine yataletwa na kamati kuu yatakayo letwa kwenye mkutano mkuu Taifa kupata baraka za mwisho kuungana.
3. Rais/ mwenyekiti aweza kuwa na kura ya turufu juu ya Jumuiya kuuungana au kutoungana na taasisi zingine.
31
38.KUVUNJIKA NA MWISHO WA JUMUIYA
Iwapo itatokea jumuiya ikavunjika au ukomo wa shughuli zake kufikia mwisho mali na amana zote za jumuiya zitagawanywa Katika mfumo ufuatao:
1: Kwa mali zote za jumuiya ambazo hazihamishiki kama ardhi nk:ambazo zimepatikana kwa njia ya umoja zitanadiwa na gawio litagawiwa kwa wanajujmuiya na ambapo wanachama ni waanzilishi watapewa zingatio la pekee.
2: Mali zingine za jumuiya ambazo zitaitwa taasisi za fedha kama mabenki ,saccos na miradi ya fedha ,zitanadiwa na kuuzwa kwa njia ya mnada na ambapo wanachama ambao ni waanzilishi /waasisi watapewa gawio la pekee.
3: Mali na amana zingine za jumuiya kama taasisi za elimu ,idara za afya na maendeleo ya jamii zitataifishwa na ambapo baraza la wazamini la jumuiya na vyombo vya dola vya serikali zitasimamia zoezi la kurithisha mali hizo kwa serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania.
4: Katika zoezi la kunadi na kutaifisha mali na amana zilizokuwa za jumuiyia ya vijana wasomi Tanzania ni vyema na muhimu baraza la wadhamini la jumuiya litapewa zingatio la juu kwenye kuratibu na kusimamia kunadi na kutaifisha mali na amana zote pamoja na serikali































No comments:

Post a Comment